Msanii wa muziki nchini Tanzania Nuh Mziwanda, baada ya kuvuka kiunzi cha skendo ya kumpachika mimba binti na kumkana hadharani, jambo ambapo lilipelekea msukosuko katika penzi lake na mpenzi wake Shilole, hatimaye atamka hadharani mipango yake ya kuazaa na Shilole.
Akihojiwa na eNews ya EATV Mziwanda amesema kuwa yeye na Shilole, wanapenda sana kupata mtoto wao, ila anafahamu kuwa hiyo ni mipango ya Mungu na wakati wowote kutoka sasa ikitokea baraka hiyo watafurahi.
Amedai kuwa Mungu akiwajalia kuwa na mtoto furaha yao itaongezeka kwa kuwa kila kitu Mungu ndio mpangaji na kusema kuwa bado yupo kwenye mipango ya ndoa baada ya kutambulishana kwa wazazi.
