Welcome

    Featured Posts

    BURUDANIKA BLOG - KWA MICHEZO NA BURUDANI ZOTE

    .

Loading...

NASH MC: HIP HOP INAPESA SANA, WANAOSEMA HAINA PESA HAWANA UTAFITI, PIA SERIKALI ICHUKUE KODI KWA WASANII ILI KUI RASMISHA SANAA KAMA AJIRA.


Hip hop ni maisha ya watu ambao wanaishi katika misingi fulani ya maisha. Kila tunachokifanya katika maisha ni misingi ya Hip Hop. Ameyaongelea hayo Nash MC wakati akihojiwa na kituo cha redio cha E FM hapa Dar es salaam.
Nash MC ameonekana kuchukizwa sana na watangazaji ambao wanapotosha misingi ya Hip Hop pia kutopendelea kuzicheza nyimbo za mtindo huu kwani DJs wengi hupendelea kucheza ngoma wazipendazo tu na zinazovuma sana kwa wakati huo bila kujua kuwa Hip Hop ni moja tu na wala haibadiliki tofauti na Bongo Flava ambayo hubadilika badilika.

“Hata ukienda German utakuta Hip Hop ile ile isipokuwa lugha tu, Ufaransa pia wataimba kwa Kifaransa Hip Hop ile ile”, alisisitiza.

Pia ameongelea kuhusiana na serikali kukosa mapato kutokana na kazi za wasanii, alisema, “Mimi nimeshawahi kutengeneza mixtape yangu na nikaiuza nikapata pesa nzuri lakini sikulipia kodi, na hakuna mtu aliyenifuata kuulizia suala lolote la kodi kutokana na kazi yangu”. Hata hivyo alisisitiza kuwa serikali ndo yenye makosa kwani ingeweza kuirasmisha sanaa na kuweza kuwatoza kodi wasanii, pesa ingepatikana nzuri. Kungekuwepo na TIN maalumu kwa wasanii na wangekuwa wanalipia kodi kubwa. Ametoa mfano Marekani kuna wasanii wengi utawasikia au kuwasoma mitandaoni kuwa wanadaiwa kodi kiasi Fulani tofauti na hapa kwetu Bongo.


SUALA LA SHOW ZAKE PIA KIPATO
Kuhusiana na maslahi anayopata, amesema kuwa show moja anaweza kupata hata milioni mbili na nusu. Hajazungumzia kiundani suala la kipato chake kwa ujumla.

MADAWA YA KULEVYA NA HIP HOP
Ameulizwa swali la kizushi kuwa, wasanii wengi wa Hip Hop wanatumia mihadarati, yaani Hip Hop inaenda samba samba na Madawa ya kulevya. “Kwanza neno stress lifutike kwa kisingizio kwamba msanii wa Hip Hop ni lazima atumie madawa ya kulevya ili kuondoa stress, ni uongo kwani tunawaona wengi tu ambao si wana Hip Hop wanatumia sana, lakini kutumia madawa ya kulevya ni mtu mwenyewe na si sanaa anayokuwemo”.

WITO KWA WANA HIP HOP
Ametoa wito kwa wana Hip Hop wenzake kuwa waangalie pale wanapokosea na waweze kuparekebisha.  “Wakae na kujiuliza ni wapi wamekosea…”. Pia ametoa maneno ambayo wana Hip Hop wote wakifuata watafanikiwa, “Peace, Love, Unity and Happiness”.


NENO KWA WATANGAZAJI
“Watangazaji wengi huenda wamewekwa kiundugu undugu tu na hawawezi kudadavua vilivyo kuhusiana na kitu Fulani hasa Hip Hop, wanacheza miziki ya washikaji wao na kusahau kugonga ngoma zilizoenda kidato.  Mara utawasikia wanasema Hip Hop hailipi, jamani Hip Hop inalipa. Mimi nawaambia hivi, NO RESEARCH NO RIGHT SAY”
© Copyright BURUDANIKA BLOG
Back To Top